Luke 6:12-16

12 aIkawa katika siku hizo Isa alikwenda mlimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu. 13 bKulipopambazuka, akawaita wanafunzi wake, naye akachagua kumi na wawili, ambao pia aliwaita mitume: 14 cSimoni aliyemwita Petro, Andrea nduguye, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo, 15 dMathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni aliyeitwa Zelote, 16Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Iskariote ambaye alikuwa msaliti.

Isa Aponya Wengi

(Mathayo 4:23-25)

Copyright information for SwhKC